Pages

Friday, 21 November 2014



ARSENAL KUFUTA UTEJA?

Na Abdul Rutona. (Msanifu wa Habari)

Kuelekea mtanange wa mahasimu katika Ligi Kuu ya Uingereza hapa kesho kati ya Arsenal na Manchester United, mengi yamesemwa na yanaendelea kusemwa hasa kwa washabiki wa timu hizo kubwa mbili zilizo na idadi kubwa ya washabiki ulimwenguni kote.

Washabiki wa Arsenal wengi wamekuwa na hamasa na kikosi chao cha mwaka huu wakichagizwa na kiwango kizuri cha Alexis Sanchez na Danny Welbeck huku washabiki wachache bado hawaamini kama kikosi chao cha mwaka huu ni imara.

Kwa upande wa Manchester United, washabiki wa timu hii wengi hawafurahishwi na kiwango cha timu yao japo wana wachezaji wenye kujitoa kama Wayne Rooney na Angel Di Maria ila wachache bado wanaamini kuwa pamoja na timu kutokuwa kizuri, vijana wa Wenger wataendelea kukaa kama kawaida. Dakika tisini za mchezo huo ndizo zitakazoamua nani mbabe siku hiyo ya Jumamosi tarehe 22 – 11 – 2014 pale kwenye uwanja wa Emirates utakaochezeshwa na Mwamuzi Mike Dean kama Mwamuzi wa Kati. 

Katika kukutana na waandishi wa habari, makocha walitoa mitazamo yao kuhusiana na mchezo huo na kutoa maendeleo ya machezaji walio na majeruhi. Kwa upande wa Wenger alisema watu wasiangalie nafasi za timu hizo katika msimamo bali waangalie uwezo wa wachezaji katika timu hizo na kubashiri kuwa mechi itakuwa nzuri kwa kutazamwa. Kocha pia alitoa habari za maendeleo za wachezaji waliokuwa na majeraha. Alisema mshambuliaji wao Olivier Giroud amepona na amekuwa akifanya vizuri hata kwenye mazoezi, pia nahodha wao Mikel Arteta naye anatarajia kuwepo. Aliendelea kutoa taarifa kuwa mabeki Laurent Korcielny, Mathieu Debuchy, golikipa David Ospina na kiungo Abou Diaby wataendelea kutokuwepo. Pia Danny Welbeck aliyeonekana kuumia katika timu ya taifa, ataangaliwa kama atawezacheza.

Kwa upande wa Machester United, Kocha Van Gaal amesema kuwa atawakosa Marcos Rojo, Phil Jones, Jonny Evans, Rafael na Falcao. Daley Blind pia natajiwa kukosa mchezo huo baada ya kuuumia kwenye mechi kati ya timu yake ya Taifa ya Uholanzi ilipocheza na Latvia. Kwa upande wa Luke Shaw, Angel Di Maria, Michael Carrick na golikipa De Gea wanawezarudi baada ya kupata matatizo madogo madogo.

Kuelekea mchezo huo, inaonesha vijana wa Wenger wamekuwa kidogo wanyonge wanapokutana na vijana wa Manchester United. Katika mechi 11 zilizopita, Arsenal wameshinda mechi moja, wametoa sare mechi tatu na kufungwa mechi 7. Mara ya mwisho vijana hawa wa Wenger kushinda ilikuwa mwaka 2011 kwa goli moja la Aaron Ramsey. Na mechi iliyoisha kwa magoli mengi ni ile ya Tarehe 28 – 08 – 2011 iliyomalizika kwa Arsenal kufungwa magoli manane kwa mawili.

Uwezekano wa wachezaji 11 watakaoanza:-


 

Historia itabaki historia, rekodi hutengenezwa na huvunjwa. 

KILA LA KHERI.